dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, July 29, 2014

Baraza la eidul Fitr Salama Hall Bwawani




Baadhi ya Wananchi na Waislamu wasikiliza hotuba iliyotolewa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,katika kusherehekea Sikukuu yaEid el Fitri, [Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
Wananchi mbali mbali wakike na wakiume wakiwa katika Ukumbi wa Salama Hall Bwawani Hotel Mjini Zanzibar wakati sherehe za Baraza la EId el Fitri lililohutubiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika kusherehekea Sikukuu ya Eid el Fitri baada ya kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, [Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake kwa Wananchi na Waislamu katika Baraza la Eid El Fitri lililofanyika leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
 Baadhi ya Viongozi na wageni mbali waliohudhuria katika sherehe za Baraza la Eid el Fitri wakiangalia na kusikiliza Hotuba iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]

  Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akiwaongoza wake mbali ,mbali wa Viongozi wa Kitaifa pamoja na wananchi  waliohudhuria katika sherehe za Baraza la Eid el Fitri wakielekea   kupata viburudishaji baada ya kumalizika kwa Hotuba   iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein  katika ukumbi wa Salama Hall Bwawani Mjini Unguja leo. [Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Sheinakisalimiana na wake wa Viongozi (pichani) akipena mkono na Mama Fatma Karume,(kulia) akiwepo na Mama Mwanamwema Shein katika viwanja vya ukumbi wa Salama Hall Bwawani Mjini Zanzibar,(wa pili kushoto) Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]

source: ZanziNews

No comments :

Post a Comment