dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, October 23, 2014

Balozi Seif Azindua Safari za Ndege ya FlyDubai kutoka Dubai hadi Zanzibar.

Wasanii wa DMCA, wakitowa burudani wakati wa Uzinduzi wa Safari ya Ndege ya Shirika la Ndege la Fly Dubai iliozinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibare Balozi Seif Ali Iddi iliofanyika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Ndege ya Shirika la FlyDubai ikiwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume tayari kwa Uzinduzi wake uliofanywa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,Itaaza safari zake moja kwa moja kutoka Dubai hadi Zanzibar na ina uwezo kuchukua Abiria 240.  


Wafanyakazi wa FlyDubai wakiwa tayari kuipokea ndege yao ikitokea Dubai wakiwa na maua kwa ajili ya uzinduzi huo. uliofanyika Zanzibar. 




Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi,akiwa na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Kimataifa ya Flydubai Bwana Sudhir Sreedhara aliyevaa miwani wakiangalia burdani ya ngoma ya Msewe Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar mara baada ya ndege ya Kampuni hiyo kutua kuanzai safari zake kati ya Dubai na Zanzibar.

Abiria wa Kwanza wa ndege ya Fly Dubai wakishuka katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar wakati ndege hiyo ilipotuwa kwa mara ya kwanza Zanzibar kwa ajili ya kuzindua Safari zake Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akizindua Safari za Ndege za Kampuni ya FlyDubai itakayo toa huduma za moja kwa moja kutoka Dubai hadi Zanzibar, inayotarajiwa kuaza hivi sasa kwa safari zake hizo, Balozi Seif akizungumza katika hafla hiyo iliofanyika katika viwanja vya ndege vya Zanzibar.


                Waheshimiwa wakifuatilia hala ya Uzinduzi wa Ndege ya Fly Dubai.

Naibu Waziri wa Wizara ya Miundombinu na Mawasaliano Zanzibar Mhe. Issa Gavu, akizungumza wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika viwanja vya ndege vya kimataifa vya Abeid Amani Karume Zanzibar.


Makamu wa Rais wa Kampuni ya Flydubai Bwana Sudhir Sreedhara, akiwahutubia wananchi waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Safari za ndege za Shirika kla ndege la FlyDubai, zilizofanyika katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.

Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu nsa Mawasiliano Zanzibar Dk. Juma Akili, akizungumza wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi wa safari za ndege ya FlyDubai. Zanzibar. 

Viongozi wa Serekali wakihudhuria katika hafla ya Uzinduzi wa Ndege ya Shirika la Ndege la Fyl Dubai uliofanyika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani KarumeZanzibar. iliozinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.


Baadhi ya wageni waalikwa katika sherehe za hafla ya Uzinduzi wa Safari ya Ndege ya Fly Dubai  iliofanyika katika uwanja wa ndege Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Flydubai Bwana Sudhir Sreedhara akimkabidhi zawadi ya Jahazi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, watika hafla ya uzinduzi wa safari za ndege za Kampuni ya FlyDubai,kati ya Dubai na Zanzibar.kulia kwa Balozi Seif ni Naibu Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar Mh. Issa Haji Ussi Gavu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akimkabidhi zawadi ya Mlango wa Zanzibar Makamu wa Rais wa Kampuni ya FlyDubai Bwana,Sudhir Sreedhara wakati wa hafla ya uzinduzi wa safari za ndege za Kampuni ya FlyDubai, zilizofanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Serikali na wea Kampuni ya FlyDubai, kutoka kushoto Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Pandu Ameir Kificho, Balozi Mdogo wa Tanzania Dubai.Mhe.Omar.Mjenga, Makamu wa Rais wa Flydubai Bwana Sudhir Sreedhara, Balozi Seif Ali Iddi, Naibu Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Mhe. Issa Haji Gavu, Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Dk.. Juma Malik Akili na ni Mratibu wa Kampuni ya Kimataifa ya usafiri wa anga ya Flydubai Bwana Riyaz Jamal.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,akimuonesha jengo jipya la abiria katika uwanja huo,Makamu wa Rais wa Flydubai Bwana Sudhir Sreedhara wakati wa hafla ya uzinduzi wa ndege hiyo uliofanyika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar. Mratibu wa Kampuni ya Kimataifa ya usafiri wa Anga ya Flydubai Bwana Riyaz Jamal.
Balozi Seif akimpongeza Makamu wa Rais wa Flydubai Bwana Sudhir Sreedhara kwa auwamuzi wa kampuni yake kutoa huduma za usafiri wa ndege kati ya Dubai na Zanzibar.Kati kati ni Mratibu wa Kampuni ya Kimataifa ya usafiri wa Anga ya Flydubai Bwana Riyaz Jamal.na kushoto Balozi Mdogo wa Tanzania Dubai Balozi Omar Mjenga.
Makamu wa Rais wa Flydubai Bwana Sudhir Sreedhara akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar wakati wa kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa safari ya ndege ya kampuni ya FlyDubai itakayoaza safari zake moja kwa moja kutoka Dubai hadi Zanzibar kwa bei rahasi kwa wateja wake kupata fursa kusafiri na ndege zao kwa bei nafuu na huduma bora.kulia ni Balozi Mdogo wa Tanzania Dubai Balozi Omar Mjenga.
Chanzo: ZanziNews

No comments :

Post a Comment