dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, April 27, 2015

Ikulu kimya kuhusu Mnikulu Gurumo.

Mnikulu, Shaban Gurumo.
Siku 51 baada Mnikulu, Shaban Gurumo, kukiri mbele ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma kupokea mgawo wa zaidi ya Sh. milioni 80.8 kutoka kwa mmiliki wa kampuni ya VIP Engineering and Marketing, James Rugemalira, hadi leo anaendelea kukalia ofisi ya umma bila kuchukuliwa hatua. 
 
Fedha hizo ni sehemu ya zaidi ya Sh. bilioni 200 zilizochotwa kifisadi katika akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
 
Mamlaka za juu serikalini ikiwamo Ikulu zimeshindwa kueleza sababu za kutomchukulia hatua za kinidhamu, ikiwamo ya kumsimamisha kazi.
 
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (pichani), lakini alisema Gurumo hayumo katika mamlaka yake ya nidhamu, bali Katibu Mkuu Ikulu ndiye anayeweza kuulizwa.Jana gazeti hili lilimtafuta Katibu Mkuu wa Ikulu, Dk. Peter Ilomo, ambaye alisema hausiki kumchukulia hatua Gurumo.
 
“Mimi sihusiki kabisa katika suala hilo, hata ukiangalia muundo wa utawala Ikulu utaona dhahiri kuwa sihusiki katika hilo, wewe tafuta muhusika atakupa majibu, ila yupo muhusika,” alisema Ilomo bila kutaja mhusika ni nani.
 
Gurumo ambaye alikiri mbele ya Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma iliyokuwa inaongozwa na Jaji Hamisi Msumi, alidai  kuwa Rugemalira ni rafiki yake takriban miaka 10 sasa, na ndiye aliyemshauri kufungua akaunti kwenye Benki ya Biashara ya Mkombozi, tawi la St. Joseph, jijini Dar es Salaam, kabla ya kumuingizia Sh. 80, 850,000 katika akaunti hiyo.
 
Kutokana na hali hiyo,  Baraza lilieleza kuwa Gurumo alikiuka sheria ya maadili ya viongozi wa umma inayokataza kiongozi wa serikali kupokea zawadi zaidi ya zawadi ndogondogo na ukarimu wa kawaida.
 
Pia, inakataza kiongozi wa umma kudai, kuomba au kupokea maslahi ya kiuchumi zaidi ya ukarimu wa kawaida au zawadi ndogondogo.
 
Hata hivyo, Gurumo aliliambia Baraza kuwa hakutambua kusudio la Rugemalira kumuwekea fedha hizo kwenye akaunti hiyo.
Alidai anahisi pengine Rugemalira alifanya hivyo kwa kuwa kipindi hicho alikuwa ana mgonjwa anayesumbuliwa na maradhi ya saratani.
 
Gurumo ambaye alikuwa anajitapa kuwa anazo fedha nyingi sana, aliendelea kudai kuwa hakujishughulisha kabisa kuuliza ili kujua sababu za Rugemalira kumuwekea fedha hizo kwenye akaunti yake. Machi mwaka huu, aliyekuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita), Philip Saliboko alisimamishwa kazi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba kwa tuhuma ya kupokea fedha Sh. milioni 40.4 katika mgawo wa Escrow.
 
Kadhalika Desemba 23, mwaka jana aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisimamishwa na balozi Sefue.

CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment