dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, August 23, 2016

Mgomo wa kisiasa ulivyomrejesha kwenye umaskini mjasiri amali mwanamke kisiwani Pemba

  • Kwa siku akivuna shilingi 150,000 sasa hazidi shilingi 5000
Na Haji Nassor, Pemba

“MIMI na umaskini tulishaachana kitambo, lakini sasa naurejea taratibu maana…!!!!...’’,aliniambia mwanamke huyo huku akipata kigugumizi.

Ni mcheshi na mchangamfu wakati wote na hasa anapokuwa kwenye biashara yake ya duka la vinywaji na vyombo vya matumizi ya nyumbani eneo la Wawi wilaya ya Chakechake ndani ya kisiwa cha Pemba.

Siti Rashid Salim (39), ambae kwa sasa ni ameshatalikiwa na aliekuwa mume wake miaka minne iliopita, aliamua kujiingiza kwenye biashara ya duka akiamini kuwa huko ataagana na umaskini.

“Naam biashara ya vyombo, juisi, soda na vitafunwa ilinikubwali kisawa sawa na mimi nilishaagana na umaskini, na maisha yangu yalikuwa juu na nikawa mwanamke wa kutegemewa na familia’’,anihadithia.

Siti alienza biashara hiyo miaka minne iliopita, alilinunua duka hilo kutoka kwa mwanajeshi mmoja, ambae yeye alipata uhamisho na kuhamia kisiwani Unguja kikazi.

Ndipo alipojitokeza yeye kuchukua nafasi ya kuendeleza duka hilo, na kujikusanyia idadi ya wateja wafikao 40 wa siku moja, na wakati akifunga duka mishale ya saa 3:30 usiku mapato hakuyaamini.

“Mimi ilikuwa nahesbu mauzo, na kisha najikuta na shilingi 150,000 hadi shiingi 160,000 na hapo sasa familia ilianza kuniangalia kwa jicho la utajiri’’,alifafanua.


Nikizungumza nae kwenye duka lake eneo la Wawi, kwa muda wa saa moja bila ya kupokea mteja kutokana na kugomewa kwa sababu ya chama anachokishabikia, anasema sasa yeye na umaskini yuko karibu mno mithili ya meno na ulimi.

“Ahaa…duka limekuwa limejaa hadi bidhaa nyengine kama chupa za chai zilikuwa nimezipanga chini hadi nje barazani, sasa unaona kama lililoingia moto, hakuna liwalo na umaskini umeshanipiga mbeleko’’,alinieleza kwa huzuni.

Ubeleko kwa Pemba ni mtu kumchukua na kumuweka mgongoni, ndiovyo mjasiriamali huyu, anavyojifafanisha yeye na kurejea tena kwenye umaskini, baada ya kubaguliwa na wanakijiji wenzake.Kwenye biashara yake hiyo mchanganyiko, alininong’neza kwa sauti nyembamba kuwa, uuzaji wa kinywaji cha juisi pekee ya matunda aliokuwa akiitengeneza mwenyewe, akiuza kati ya shilingi 35,000 hadi shilingi 40,000 kwa siku moja.

Kumbe ndoo nne za juisi kwa wakati huo kabla ya kugomewa, zilimtosheleza kumuda gharama za kodi ya mlango, ambao ni shilingi 40,000 kwa mwezi mmoja.

Lakini sasa kutokana na kuteswa na wanakijiji wenzake kwa kutomnulilia bidhaa zake, na kuanza kujihesabu anaerudia kwenye dimbwi kama sio mto wa umaskini, ana deni la mezi sita la kodi ya mlango.

“Hivi sasa mwenye mlango juzi kaja kunikumbusha deni la mwezi Disemba mwaka 2015 hadi Aprili mwaka 2016, sijamlipa, lakini kanipa tena muda’’,alinionyesha mkataba wake mwanadada huyo.

Kumbe mwanamke huyu mfanyabishara, ikifika mwezi Oktoba mwaka huu, atakuwa ameshajikusanyia deni la kodi ya mlango la mwaka mmoja, la shilingi 480,000 sawa na shilingi 240,000 kwa kila miezi sita.

Nilipotaka kufahamu mauzaji yake kwa siku, ili amudu gharama walau za kodi ya mlango na yeye kujipatia mahitaji yake kwa siku, alisema hilo kwa sasa ni gumu.

Maana kabla ya kususiwa na wateja wake ambao wengi wako vyama tofauti na yeye, alikuwa akiiuza wastani wa shilingi 150,000 hasi shilingi 160,000 ambapo kwa sasa hazidi shilingi 5000 kutoka asubuhi anapofungua hadi usiku.

“Sasa biashara yangu imekufa mwandishi, nakushuruku wewe kuninunulia hiyo soda ya shilingi 600, na mauzo yangu jana yalipanda kutoka shilingi 5,000 za kawaida hadi shilingi 5,500 tu’’,alinieleza siku ya pili yake baada ya mahojiano haya.

Ukifika ndani ya duka lake lililo nje kidogo ya mji wa Chakechake, utakaribisha na nyuzi nyuzi alizokuwa akifungia biashara za kuning’nia sambamba na femu za vyakula zikiwa tupu.

Ukandamiziaji kama sio udhalilishwa kwa mwanamke huyu anaofanyiwa anasema haoni msaidizi walau kama vyombo vya haki za binadamu wala viongozi wa dini.

Sas anafungua duka hilo sio wakati wa kawaida, wala kwa ajili ya kujipatia kipato, bali ni baada ya kumaliza shughuli zake za nyumbani, na hufanya kama sehemu ya mapunziko tu.

“Silifungi duka hata kama hawaninunulii, maana nikimaliza kazi za nyumbani hujazangu hapa kama kijiweni kwangu, na walau kutia chaji simu yangu’’,alisema kwa huzini sana.

Siti ambae ni mjane, anaeishi na mama yake wa kambo na baba yake mazazi akiwa na watoto watano, wanaomtegemea anahisi dunia na walimwengu kama waliomuinamia kwa kukumba na hali ngumu ya maisha.

Ndani ya duka laki hilo ambalo liko pacha na mwenzake mmoja ambae yeye hana shida na wateja, anasema zipo bidhaa kama sahani za kigae, sabuni za unga, soda, juisi zimeshakaa kwa muda bila ya kununuliwa jambo analolitarajia kumuongezea hasara.

“Sahani sasa nazishusha bei kutoka shilingi 3,000 na sasa shilingi 2,000 na nashukuru mwandishi walau umenunua sahani nne, lakini sijui hizi nyengine na vikombe nizifanye nini’’,aliniambia akitiriri maneno ya huzuni.

Kwani wateja wako unategemea wakaazi wa hapa kijiji cha Mbuni shehia za Wara na Wawi pekee, nilimuuliza na kujibu kuwa hata wapita njia, lakini hao ndio wachache sana.

Kutokana na kukataliwa na wateja wake kwa sababu ya kushiriki uchaguzi wa marudio wa Mchi 20, mwaka huu anaona dhahiri malengo ya kujenga nyumba yake ya kudumu yamepotea.

“Unajua malengo kwanza ni kujenga nyumba yangu, ili tusisongamane kwenye myumba ya familia na kisha kukuza biashara ili niuze kwa jumla, lakini sasa wapi nimerudi nyuma’’,anasema kwa uchungu.

Pamoja na kuambiwa uso kwa uso na baadhi ya watu kwamba amegomewa lakini mwezi wa Machi mwaka huu alibandikiwa karatasi ikitoa onyo kwamba kusiwe na mtu atakae mnunulia mfanyabiashara.

Tangaazo si ruhusa mtu yoyote kutumiya dula la siti atakaeonekana kazi kwake’ ilieleza karatasi aliobandikiwa kwenye mlango wake wa duka na kuamua kukihifadhi hadi leo.

Anasema wapo watu wa familia yake wamekubaliana na wanakijiji kumgomea kwenye biashara, ingawa anadhani kwenye harusi na misiba wanaweza kushiriki.

“Sijapa harusi wala msiba tokea umalizike uchaguzi wa marudio, lakini sidhani kuwa hawatashirikiana na mimi, wao zaidi ni kwenye biashara maana lengo mpaka nihame’’,alifafanua.

Mmoja wa wazazi wake ambae alisema asitangaazwe jina lake, alikiri kuwa mtoto wao alishaanza kuwaonyesha njia ya kupunguza ukali wa maisha.

“Unajua mwandishi ndani mwetu ilikuwa tukihitaji sabuni au kitoweleo lazima tukutane, lakini biashara ilipokuwa imemkubali mtoto wetu Siti, wala hatukuwa na shida’’,alisema mzazi huyo.

Anazidi kunihadithi kuwa, hata eneo la kujenga nyumba ya kudumu kwa mtoto wao walishakuwa nalo kwa ajili yake, lakini kutumia demokrasia yake Machi 20 ndio matokeo yake hayo.

“Sisi hatuachana na chama chetu cha CCM kwa sababu wengine tu hawapendi, wao wanachama chao na sisi tuna chetu, sasa vyama na biashara havina uhusiano, maana vipo vingi kusudi mtu achague atakacho’’,alisema.

Mmoja kati yavijana wanaoishi mtaani hapo Ali Mohamed ambalo sio jina lake rasmi, alinieleza kuwa kulikuwa na kikao maalumu kwa kila mtu hata awe CUF, ADC, CCM, CHADEMA akishiriki uchaguzi wa marudio atengewe.

Lakini mwanamke mmoja (45) wa kijiji hicho anasema hata wao walitakiwa wasinunue bidhaa kwenye duka la Siti, ingawa hawakubaliana na wazo hilo.

Wamekuwa wakitamani sana kumnunulia bidhaa mwanamke mwezao, ingawa wanahofu ya kutengwa na wao na wakijiji kama agizo lilivyotoka.

Nilitaka kujua kwa ndani juu ya hili, nilimtafuta Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Chakechake Saleh Nassor Juma, na kuthibitisha kuwa ndio agizo la baraza kuu la Chama kutoshirikiana na mwanaCCM.

“Unajua yaliojitokeza Oktoba 28 mwaka jana kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi, sasa CUF iliazimia hata mwanachama wake akishirikia uchaguzi wa marudio, basi nae atengwe na hayo yanayowakumba wenye biashara’’,alifafanua.

Yussuf Ali Juma yeye ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Chakechake anaelewa vyema mateso yanayoendelea kuwapata mwanachama wao kwa kugomewa biashara zao na shughuli za kiutu.

“Sisi kama CCM twaseme hili wanalofanyiwa wanachama wetu, sio siasa tene ni ukiukwaji wa haki za binadamu, lakini naamini yatakwisha siku moja’’,alieleza.

Anasema wanachofikiria ni kuangalia uwezekano wa mwanachama wao Siti kuhamia eneo jengine kibiashara ili ajikombowe na umaskini kama akihisi eneo alillo linaendelea kumpotezea malengo.

CCM inaendelea kushangaa kilichowakuta wanaowanachama wao zaidi ya 16, waliokumbwa na mkasa wa kupewa talaka kwa sababu ya kushiriki uchaguzi wa marudio.

Lakini Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania ofisi ya Zanzibar TAMWA kupitia Mratib wake Mzuri Issa, hivi karibuni akizungumza na vyombo vya habari, alisema lazima udhalilishaji wa aina hii upigwe vita.

“Mwanamke kumzuilia kushiriki uchaguzi, au kumlazimisha kuchagua kiongozi anaetaka mwanamme au kumsusia kwa sababu ya kutumia demokrasia yake ni udhalilisha mkubwa na haufai’’,alisisitiza.

Haki ya kupiga kura, ambayo ni haki ya kikatiba kwenye kifungu cha 7, cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, bado inaendelea kulitesa kundi la wanawake hapa Zanzibar.

Huku baadhi ya wanaharakati wa masuala ya kutetea haki za wanawake na watoto, wakiwataja baadhi ya wanaume waliokwenye ndoa kuyatumia vibaya madaraka yao.

/ZanziNews.

No comments :

Post a Comment